Tanzania National Parks (TANAPA) is a Parastatal Organization whose mandate is to manage and regulate the use of areas designated as National Parks. The Organization currently manages twenty-two National Parks which form part of larger protected ecosystems set aside to preserve Tanzania’s rich natural heritage.
 


TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI


Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) anapenda kuwataarifu waombaji kazi wote walioomba kazi zilizotangazwa  kwa  niaba  ya  Mamlaka  hiyo  kuwa  usaili  unatarajiwa  kuendeshwa kuanzia tarehe 25 - 29 Januari, 2022 katika Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Oljoro Arusha na hatimaye kuwapangia vituo vya kazi waombaji kazi watakaofaulu usaili.

Wasailiwa wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:-

i.      Usaili utafanyika    tarehe  25-29  Januari, 2022  katika  Kambi ya  Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Oljoro Arusha kama ilivyooneshwa kwenye tangazo hili; muda na tarehe ambapo usaili utafanyika umeainishwa kwa kila msailiwa;
ii.     Wasailiwa wote wanapaswa kuripoti katika Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Oljoro Arusha tarehe 24 Januari, 2022 ambapo huduma zote za chakula na malazi watapatiwa bila malipo wakiwa kambini;
iii.    Usaili wa Vitendo utafanyika kuanzia tarehe 25-27 Januari, 2022;
iv.    Usaili wa Mahojiano ya ana kwa ana utafanyika tarehe 29 Januari, 2022;
v.     Kila  msailiwa  anatakiwa  kufika  kwenye  eneo  la  usaili  akiwa  amevaa barakoa, kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka ama kutakasa mikono;
vi.    Kila   msailiwa   anapaswa   kuwa   na   kitambulisho   kwa   ajili   ya   utambuzi; vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:- Kitambulisho cha Mkazi, Kitambulisho cha Mpiga kura, Kitambulisho cha kazi, Kitambulisho cha Uraia au Hati ya kusafiria;
vii.   Wasailiwa wanatakiwa kufika na VYETI VYAO HALISI, kuanzia cheti cha kuzaliwa, kidato cha IV, VI, Stashahada, Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea kutegemeana na sifa za Mwombaji;
viii. Wasailiwa  watakaowasilisha  “Testimonials”,  “Provisional  Results”, “Statement of results”, hati za matokeo za kidato cha IV na VI (form V and form VI results slips) HAVITAKUBALIWA NA HAWATARUHUSIWA KUENDELEA NA USAILI;
ix.    Kila Msailiwa azingatie tarehe, muda na mahali alipopangiwa kufanyia usaili;
x.     Kwa waombaji      waliosoma    nje   ya   Tanzania   wahakikishe   Vyeti   vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (kama TCU, NACTE au NECTA);
xi.    Waombaji   kazi   ambao   majina   yao   hayakuonekana   katika   tangazo   hili watambue kuwa hawakukidhi vigezo.  Hivyo, wasisite kuomba tena pindi nafasi za kazi zitakapotangazwa na kuzingatia mahitaji ya tangazo husika.
xii.   Wasailiwa wote walioitwa kwenye usaili wahakikishe wanaingia kwenye akaunti  zao  na  kunakili  namba  ya  mtihani  kwa  kuwa  namba  hizo
hazitatolewa siku ya usaili.

BOFYA HAPA KUSOMA KWA UKAMILIFU TANGAZO HILI RASMI KUTOKA UTUMISHI