TANGAZO  LA NAFASI ZA KAZI
Mkurugenzi  Mtendaji  wa Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Kibondo  anakaribisha  maombi  ya  Kazi kwa nafasi zifuatazo.
1.0.    MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III- NAFASI 01
1.1.     SIFA ZA MWOMBAJI
Mwombaji anatakiwa  awe  na cheti  cha  kufaulu  Kidato  cha  Nne  na  waliohitimu  mafunzo ya          Cheti (Astashahada) katika fani zifuatazo: Utawala, Uongozi  na Usimamizi wa Fedha, Sheria, Elimu ya Jamii,  Maendeleo  ya Jamii  na Sayansi  ya Sanaa  kutoka  Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo au Chuo/Taasisi yoyote inayotambuliwa  na Serikali.
1.2.      KAZI NA MAJUKUMU
•    Kuandaa  taarifa  za  Utekelezaji  wa  kazi  katika  eneo  lake  na  kuhamasisha wananchi  katika kuandaa na kutekeleza mikakati ya kuondoa njaa, umasikini na kuongeza uzalishaji  mali.
•    Kusimamia,  kukusanya  na kuhifadhi kumbukumbu zote na nyaraka za Kijijj.
•    Kiongozi wa wataalamu  (watumishi wa serikali) katika kijiji.
•    Mhasibu  (Afisa  masuuli) na Mtendaji Mkuu wa kazi
za kila siku za Serikali ya Kijiji.
•    Kutafsiri  na kusimamia  utekelezaji  wa Sera,  Sheria  na Taratibu  zinazotolewa
na Serikali ya Jamhuri  ya Muungano  wa Tanzania.
•    Kusimamia Ulinzi  na Usalama wa raia na mali zao,  kuwa Mlinzi wa Amani  na
Msimamizi wa utawala bora katika kijiji.
•    Katibu wa Mikutano  na Kamati zote za Halmashauri ya Kijjjj.
•    Kuratibu  na kusimamia  upangaji  na utekelezaji  wa Mipango  ya Maendeleo  ya Kijii.
•    Kutekeleza  Shughuli  nyingine atakazopangiwa na Mwajiri.
•    Atawajibika kwa Mtendaji wa Kata.
1.3.      MSHAHARA
Kwa kuzingatia  viwango  vya Serikali  yaani ngazi ya Mshahara  TGS B
2.0.      KATIBU MUHTASI  Ill    - NAFASI 01
2.1.    SIFA ZA MWOMBAJI
Mwombaji anatakiwa  awe na cheti cha kufaulu  Kidato cha  Nne na waliohudhulia Mafunzo ya Uhazili  na  kufaulu  mtihani  wa  Hatua  ya  Tatu.  wawe  wamefaulu  somo   la  Hatimkato   ya Kiswahili  na  Kingereza   maneno   80  kwa  dakika   moja  na  wawe   wamepata   mafunzo  ya kompyuta    kutoka   chuo    chochote   kinachotambuliwa   na   Serikali    nakupata    cheti   katika programu za windows,  Microsoft office, Internet, Email na Publisher.
2.2.    KAZI NA MAJUKUMU
•    Kuchapa  barua,  taarifa  na nyaraka za kawaida.
•    Kusaidia    kupokea   wageni   na   kuwasaili   shida   zao,    nakuwaelekeza   sehemu wanapoweza kushughulikiwa.
•    Kusaidia  kutunza  taarifa/kumbukumbu za matukio, miadi, wageni, tarehe za vikao, safari  za Mkuu wake  na ratiba  za kazi  nyingine  zilizopangwa  kutekelezwa   katika Ofisi  anamofanyia kazi,  na kumuarifu  Mkuu wake kwa wakati  unaohitajika,
•    Kusaidia  kutafuta  na kumpatia  Mkuu wake majalada,  nyaraka  au kitu chochote kinachohitajika katika  shughuli za hapo ofisini.
•    Kusaidia  kufikisha  maelekezo  ya Mkuu wake  wa  kazi kwa wasaidizi  wake  na pia
kumuarifu  kuhusu tarifa  zozote  anazokuwa  amepewa  na wasaidizi  hao.
•    Kusaidia  kupokea  majalada,  kuyagawa  kwa  Maofisa  walio  katika  sehemu  alipo, na kuyakusanya,  uyatunza na kuyarudisha  sehemu  zinazohusika.
•    .Kutekeleza kazi zozote  atakazokuwa  atakazokuwa  amepangiwa na Msimamizi wake wa kazi
Kibondo,  SL.P 43,  Kibondo- Kigoma, Simu: +25528-2820084,  Nukustr +25528-2820084, Barua pepe: ded@ibondodc.gp.{z Tovuti: www kibondodc.go.t2
[Barua zote ziandikwe kwa Mkurugenzi Mtendaji (W)]
2.3.      MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango  vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara  TGS  B
2.4. MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI
• Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45
• Waombaji wote waambatanishe cheti cha kuzaliwa.
• Waombajj waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed CV yenye anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina y wadhamini (referees) watatu wa kuaminika.
• Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, nakala za vyeti vy Kidato cha Nne na Kidato cha Sita kwa wale waliofikia kiwango hicho n vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika.
• Picha moja "Passport size" ya hivi karibuni iandikwe jina kwa nyuma.
• Testmonials", "Provisional Results", "Statement of results", Hati za Matoke ya Kidato cha NNE na RESULTS SLIPS HAVITAKUBAULIWA.
• Maombi yanaweza kuandikwa kwa Lugha ya Kiswahili fasaha au Kingerez fasaha.
• Mwisho wa kupokea barua za maombi ni tarehe 20, Januari, 2022 saa 9:30 Alasiri na yatumwe kupitia Posta kwa anuani ifuatayo:
MKURUGENZI MTENDAJI,
HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO, S.L.P 43,
KIBONDO
IMETOLEWA NA:
Rutema D.M MKURUGENZI MTENDAJI (W) KIBONDO
Also See: Other Government Jobs Here
Check Out Other Office Administration Jobs Here
Also View: Other Jobs in Kigoma Here
