Ticker

Welcome

Tangazo la Nafasi 2 za Kazi Kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo , Kigoma

 

TANGAZO  LA NAFASI ZA KAZI  Mkurugenzi  Mtendaji  wa Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Kibondo  anakaribisha  maombi  ya  Kazi kwa nafasi zifuatazo.


TANGAZO  LA NAFASI ZA KAZI


Mkurugenzi  Mtendaji  wa Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Kibondo  anakaribisha  maombi  ya  Kazi kwa nafasi zifuatazo.

1.0.    MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III- NAFASI 01


1.1.     SIFA ZA MWOMBAJI

Mwombaji anatakiwa  awe  na cheti  cha  kufaulu  Kidato  cha  Nne  na  waliohitimu  mafunzo ya          Cheti (Astashahada) katika fani zifuatazo: Utawala, Uongozi  na Usimamizi wa Fedha, Sheria, Elimu ya Jamii,  Maendeleo  ya Jamii  na Sayansi  ya Sanaa  kutoka  Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo au Chuo/Taasisi yoyote inayotambuliwa  na Serikali.

1.2.      KAZI NA MAJUKUMU
•    Kuandaa  taarifa  za  Utekelezaji  wa  kazi  katika  eneo  lake  na  kuhamasisha wananchi  katika kuandaa na kutekeleza mikakati ya kuondoa njaa, umasikini na kuongeza uzalishaji  mali.
•    Kusimamia,  kukusanya  na kuhifadhi kumbukumbu zote na nyaraka za Kijijj.

•    Kiongozi wa wataalamu  (watumishi wa serikali) katika kijiji.
•    Mhasibu  (Afisa  masuuli) na Mtendaji Mkuu wa kazi
za kila siku za Serikali ya Kijiji.
•    Kutafsiri  na kusimamia  utekelezaji  wa Sera,  Sheria  na Taratibu  zinazotolewa

na Serikali ya Jamhuri  ya Muungano  wa Tanzania.

•    Kusimamia Ulinzi  na Usalama wa raia na mali zao,  kuwa Mlinzi wa Amani  na

Msimamizi wa utawala bora katika kijiji.

•    Katibu wa Mikutano  na Kamati zote za Halmashauri ya Kijjjj.

•    Kuratibu  na kusimamia  upangaji  na utekelezaji  wa Mipango  ya Maendeleo  ya Kijii.

•    Kutekeleza  Shughuli  nyingine atakazopangiwa na Mwajiri.
•    Atawajibika kwa Mtendaji wa Kata.

1.3.      MSHAHARA
Kwa kuzingatia  viwango  vya Serikali  yaani ngazi ya Mshahara  TGS B


2.0.      KATIBU MUHTASI  Ill    - NAFASI 01



2.1.    SIFA ZA MWOMBAJI

Mwombaji anatakiwa  awe na cheti cha kufaulu  Kidato cha  Nne na waliohudhulia Mafunzo ya Uhazili  na  kufaulu  mtihani  wa  Hatua  ya  Tatu.  wawe  wamefaulu  somo   la  Hatimkato   ya Kiswahili  na  Kingereza   maneno   80  kwa  dakika   moja  na  wawe   wamepata   mafunzo  ya kompyuta    kutoka   chuo    chochote   kinachotambuliwa   na   Serikali    nakupata    cheti   katika programu za windows,  Microsoft office, Internet, Email na Publisher.

2.2.    KAZI NA MAJUKUMU

•    Kuchapa  barua,  taarifa  na nyaraka za kawaida.

•    Kusaidia    kupokea   wageni   na   kuwasaili   shida   zao,    nakuwaelekeza   sehemu wanapoweza kushughulikiwa.
•    Kusaidia  kutunza  taarifa/kumbukumbu za matukio, miadi, wageni, tarehe za vikao, safari  za Mkuu wake  na ratiba  za kazi  nyingine  zilizopangwa  kutekelezwa   katika Ofisi  anamofanyia kazi,  na kumuarifu  Mkuu wake kwa wakati  unaohitajika,
•    Kusaidia  kutafuta  na kumpatia  Mkuu wake majalada,  nyaraka  au kitu chochote kinachohitajika katika  shughuli za hapo ofisini.
•    Kusaidia  kufikisha  maelekezo  ya Mkuu wake  wa  kazi kwa wasaidizi  wake  na pia

kumuarifu  kuhusu tarifa  zozote  anazokuwa  amepewa  na wasaidizi  hao.

•    Kusaidia  kupokea  majalada,  kuyagawa  kwa  Maofisa  walio  katika  sehemu  alipo, na kuyakusanya,  uyatunza na kuyarudisha  sehemu  zinazohusika.
•    .Kutekeleza kazi zozote  atakazokuwa  atakazokuwa  amepangiwa na Msimamizi wake wa kazi
Kibondo,  SL.P 43,  Kibondo- Kigoma, Simu: +25528-2820084,  Nukustr +25528-2820084, Barua pepe: ded@ibondodc.gp.{z Tovuti: www kibondodc.go.t2
[Barua zote ziandikwe kwa Mkurugenzi Mtendaji (W)]
2.3.      MSHAHARA

Kwa kuzingatia viwango  vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara  TGS  B




2.4.      MASHARTI YA JUMLA  KWA WAOMBAJI

•   Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45

•    Waombaji wote waambatanishe cheti cha kuzaliwa.

•    Waombajj  waambatishe  maelezo   binafsi  yanayojitosheleza  (Detailed  CV yenye  anwani  na  namba  za  simu  za  kuaminika    pamoja   na  majina  y wadhamini  (referees)  watatu wa kuaminika.
•    Maombi       yote      yaambatane  na  vyeti  vya  taaluma,  nakala  za  vyeti  vy Kidato  cha  Nne na  Kidato  cha  Sita  kwa wale waliofikia  kiwango  hicho  n vyeti vya kuhitimu  mafunzo  mbalimbali  kwa kuzingatia  sifa za kazi husika.
•    Picha moja "Passport  size" ya hivi karibuni  iandikwe  jina  kwa nyuma.

•    Testmonials",  "Provisional  Results", "Statement of results",   Hati za  Matoke ya Kidato  cha NNE na RESULTS  SLIPS  HAVITAKUBAULIWA.
•    Maombi yanaweza  kuandikwa kwa Lugha ya Kiswahili fasaha au Kingerez fasaha.
•    Mwisho  wa  kupokea  barua za maombi  ni  tarehe  20,  Januari,  2022 saa 9:30 Alasiri  na yatumwe kupitia  Posta kwa anuani  ifuatayo:


MKURUGENZI MTENDAJI,
HALMASHAURI YA WILAYA  YA KIBONDO, S.L.P 43,
KIBONDO

IMETOLEWA NA:

Rutema D.M MKURUGENZI  MTENDAJI  (W) KIBONDO

Get New Job Updates Here

Also See: Other Government Jobs Here

Check Out Other Office Administration Jobs Here

Also View: Other Jobs in Kigoma Here