TANGAZO  LA KAZI YA MHASIBU   SIFA NA UJUZI Awe na digrii katika mambo ya Fedha, Benki, Uhasibu au inayolingana  na hizo kutoka katikachuo kinachotambulikana.



TANGAZO  LA KAZI YA MHASIBU



SIFA NA UJUZI

Awe na digrii katika mambo ya Fedha, Benki, Uhasibu au inayolingana  na hizo kutoka katikachuo kinachotambulikana.


Awe na sifa za kitaaluma. (CPA, ACCA au inayolingana na hizo) na uzoefu usiopungua miaka mitatu katika mazingira ya biashara ushindani


Mwenye  uwezo  wa  kufanya  kazi  bila  ya  usimamizi  wa  karibu  na uwelewa  mzuri, mwaminifu na tabia nzuri na uzoefu wa mifumo ya Tehama  ya kihasibu ya SACCOS

Recommended for you: Get the Latest & New Job Updates Here     


KAZI NA MAJUKUMU
-    Kuhakikisha  mapato  na  matumizi  yameingizwa  katika  vitabu  vya  hesabu  kwa
usahihi..
-    Kuhakikisha  taarifa  zote  za   mikopo,  akiba,  hisa   na  amana   za  wanachama
zimeingizwa kwa usahihi kwenye leja za wanachama
-   Kuhakikisha malinganisha  ya miamala ya benki na fedha taslimu yanafanyika kila mwezi.
-   Kuhakikisha marejesho ya mikopo yanafanyika kila mwezi kulingana na jedwali la marejesho.ya kila mwanachama aliyekopa.
-    Kuhakikisha  balansi za hisa, akiba, amana na mikopo ya wanachama inalingana na
leja kuu.
-   Kutoataarifa ya hali ya mikopo, akiba na amana za wanachama  kila mwezi.
-    Kutunza daftari la kumbukumbu  za wanachama kwa usahihi (members  register)
-   Kutoa taarifa ya mikopo mibaya kila mwezi.
-   Kutayarisha taarifa ya Urari wa hesabu kila mwezi
-    Kutayarisha taarifa ya mapato na matumizi kila mwezi.
-    Kutayarisha taarifa ya mizania kila mwezi.
-   Kutayarisha taarifa ya malinganisho ya bajeti na hali halisi kila mwezi.
-   Kutayarisha taarifa ya badiliko la mtaji kila mwezi.
-   Kuandaa  taarifa  ya  mtiriko  wa fedha  kila  mwezi,  daftari la mali  za kudumu   na
mishahara ya wafanyakazi.


JINSI YA KUTUMA MAOMBI

•     Tarehe  ya mwisho ya kupokea maombi 11.02.2022 Saa 10:30 jioni.


Tuma maombi kwa barua pepe kupitia msaccos@mwananchi.co.tz
CV pamoja na vyeti

Recommended for you: Get the Latest & New Job Updates Here     


Check out Other Jobs in Dar es Salaam Here