Ticker

Welcome

Nafasi 5 za Kazi - kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa

 

TANGAZO  LA KAZI  MKURUGENZI   WA HALMASHAURI  YA  MANISPAA   YA  IRINGA ANAPENDA KUTANGAZA NAFASI ZA KAZI KWA WATANZANIA  WOTE WENYE SIFA  KAMA IFUATAVYO: •


Kumb.  Na. IMC/S.20/2/VOL.1/12 LNLU5                      Tarehe 29/12/2021

TANGAZO  LA KAZI


MKURUGENZI   WA HALMASHAURI  YA  MANISPAA   YA  IRINGA ANAPENDA KUTANGAZA NAFASI ZA KAZI KWA WATANZANIA  WOTE WENYE SIFA  KAMA
IFUATAVYO: •

1.0 DEREVA DARAJA LA II - (NAFASI 2)

1.1 MAJUKUMU  NA KAZI:

i.       Kukagua Gari kabla  na baada ya safari ili kubaini  hali ya usalama wa Gari. ii.      Kuwapeleka Watumishi  maeneo mbalimbali kwenye safari za kikazi.
iii.      Kufanya matengenezo madogo  madogo  ya Gari. iv.      Kukusanya  na kusambaza  Nyaraka mbalimbali.
v.      Kujaza  na kutunza  taarifa za Safari zote katika daftari la safari (Log book).
vi.      Kufanya  usafi wa Gari.
vii.      Kufanya  kazi nyingine kadri utakavyoelekezwa na Msimamizi wako.

1.2 SIFA ZA MWOMBAJI:

Waombaji  wawe na  Cheti  cha Mtihani wa Kidato  cha IV wenye Leseni ya  Daraja  E au  Daraja  C,  ya  uendeshaji  magari  pamoja  na  uzoefu  wa  kuendesha  magari kwa muda usiopungua  Mwaka mmoja  bila kusababisha ajali.  Awe amehudhuria  mafunzo ya msingi ya uendeshaji  magari (Basic Driving Course) yanayotolewa   na  Chuo cha  Mafunzo  ya   ufundi  Stadi  (VETA)   au  Chuo   kinachotambuliwa  na   Serikali. Waombaji wenye Cheti   cha  majaribio  ya  Ufundi  wa  Daraja  la  II watafikiriwa kwanza.

1.3  NGAZI  YA MSHAHARA
Ngazi ya Mshahara ni kwa kuzingatia viwango vya serikali yaani TGSB kwa mwezi.


2.0     MSAIDIZI  WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II - (NAFASI 1)

2.1     MAJUKUMU NA KAZI:
i.    Kutafuta  kumbukumbu/nyaraka/mafaili yanayohitajiwa  na wasomaji.
ii.   Kudhibiti upokeaji na uandikishaji wa kumbukumbu/nyaraka.
iii.  Kuchambua, kuorodhesha  na kupanga  kumbukumbu/nyaraka  katika  makundi kulingana  na somo husika (Classification and Boxing) kwa ajili ya matumizi ya ofisi.
iv.  Kuweka/kupanga  kumbukumbu/nyaraka  katika reki (file rakes/cabinets)
katika Masijala/Nyumba  vya kuhifadhia  kumbukumbu.
v.   Kuweka  kumbukumbu (barua, nyaraka nk) katika mafaili.
vi.  Kushughulikia maombi ya kumbukumbu/nyaraka  kutoka  Taasisi za Serikali.

2.2     SIFA  ZA WAOMBAJI

Waombaji wawe wamehitimu Kidato  cha nne au  cha Sita, wenye  cheti cha Utunzaji
Kumbukumbu katika mojawapo ya fani za Afya,  Masijala,  Mahakama na Ardhi.

2.3    NGAZI YA MSHAHARA
Ngazi ya Mshahara  ni kwa kuzingatia viwango vya serikali  yaani TGSB kwa mwezi.

3.0     MTENDAJI  WA MTAA DARAJA LA III - (NAFASI 2)

3.1     MAJUKUMU NA KAZI
i.     Katibu wa Kamati  ya Mtaa. ii.     Mtendaji Mkuu wa Mtaa.
iii.     Mratibu  wa utekelezaji wa Sera  na Sheria  zinazotekelezwa  na  Halmashauri katika
Mtaa.
iv.    Mshauri wa Kamati ya Mtaa kuhusu mipango ya maendeleo  katika  Mtaa.
v.     Msimamizi   wa   utekelezaji   wa    Sheria    ndogo  pamoja    na   Sheria   nyingine zinazotumika  katika  Mtaa.
vi.     Mshauri wa kamati ya Mtaa kuhusu  masuala ya ulinzi na usalama.
vii.     Msimamizi wa utekelezaji wa mikakati mbalimbali inayohusu  uondoaji wa njaa  na umaskini katika Mtaa.
viii.     Kusimamia  ukusanyaji  wa  mapato  ya  Halmashauri  na  kutunza  kumbukumbu   za walipa kodi wote.
ix.     Kuandaa na kutunza  rejesta ya wakazi wote wa Mtaa.
x.      Atawajibika  kwa Mtendaji wa Kata.

3.2     SIFA ZA WAOMBAJI

Waombaji  wawe  wamehitimu  kidato  cha  nne (IV)  au  sita (VI).  Waliohitimu mafunzo  ya  Astashahada  katika  moja  ya  fani  zifuatazo;  Utawala, Sheria,  Elimu ya Jamii, Usimamizi wa Fedha, Maendeleo  ya Jamii na Sayansi  ya Sanaa kutoka Chuo     cha   Serikali     za     Mitaa     Hombolo,      Dodoma     au   Chuo    chochote kinachotambuliwa  na Serikali.

3.3  NGAZI YA MSHAHARA
Ngazi ya Mshahara ni kwa kuzingatia viwango vya serikali  yaani TGSB kwa mwezi.

MASHARTI YA UJUMLA

i.        Mwombaji  lazima  awe raia wa  Tanzania na awe tayari kufanya kazi katika Idara yoyote atakayopangiwa.
ii,      Mwombaji awe na umri usiopungua miaka 18 na usiozidi miaka 45.

iii.      Mwombaji   aambatishe   maelezo yake  binafsi  yanayojitosheleza   (Detailed  CV)
yenye anuani na namba za simu za kuaminika.

iv.      Mwombaji  aambatishe  nakala  ya vyeti vya uendeshaji  magari (Taaluma), cheti cha Kidato cha IV, Cheti cha Kuzaliwa na picha mbili za rangi za hivi karibuni na ziandikwe majina kwa nyuma, nakala hizo zithibitishwe na Hakimu au Wakili.

v.      Mwisho wa kupokea barua za maombi  ni tarehe 11 Januari, 2022  Saa 9:30 Alasiri.

Maombi yote yatumwe kupitia anuani ya posta  kama ifuatavyo;•

Mkurugenzi wa Manispaa,
Halmashauri ya Manispaa ya Iringa,
S.LP.  162,
IRINGA.



NB: Tangazo hili linapatikana pia kwenye Tovuti ya Halimashauri ya Manispaa ya Iringa ambayo ni www.iringamc.go.tz

Bofya hapa ili kuwownload Tangazo Hili Katika Mtindo Rahisi Kuprint wa PDF
 

 
Also See: Other Government Jobs Here